Ikulu yaendelea na Mazungumzo ya Makinikia
Mazungumzo kati ya Kamati Maalum iliyoundwa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na timu ya kutoka
Barrick Gold Corporation yameendelea leo Jijini Dar es Salaam.
Mazungumzo hayo yanafanyika kufuatia uchunguzi uliofanywa na tume mbili zilizoundwa na Mhe. Rais Magufuli kuchunguza biashara ya madini ya dhahabu na kubaini uwepo wa upotevu mkubwa fedha katika biashara ya makinikia ya dhahabu ambayo husafirishwa kwenda nje ya nchi.
Wakati mazungumzo hayo yanaendelea wananchi wanataarifiwa kuwa na subira na watajulishwa mara baada ya mazungumzo hayo kukamilika ama kwa hatua yoyote itakayofikiwa.
Kamati Maalum ya Tanzania inayofanya majadiliano na timu kutoka Barrick Gold Corporation inaongozwa na Waziri wa Sheria na Katiba Prof. Palamagamba Kabudi.
Mazungumzo hayo yanafanyika kufuatia uchunguzi uliofanywa na tume mbili zilizoundwa na Mhe. Rais Magufuli kuchunguza biashara ya madini ya dhahabu na kubaini uwepo wa upotevu mkubwa fedha katika biashara ya makinikia ya dhahabu ambayo husafirishwa kwenda nje ya nchi.
Wakati mazungumzo hayo yanaendelea wananchi wanataarifiwa kuwa na subira na watajulishwa mara baada ya mazungumzo hayo kukamilika ama kwa hatua yoyote itakayofikiwa.
Kamati Maalum ya Tanzania inayofanya majadiliano na timu kutoka Barrick Gold Corporation inaongozwa na Waziri wa Sheria na Katiba Prof. Palamagamba Kabudi.

Post a Comment: