Wednesday, 22 March 2017

RIPOTI YA KAMATI ILIYOUNDWA NA WAZIRI NAPE NNAUYE KUHUSU UVAMIZI WA MEDIA-

Waziri Nape Nnauye anapokea taarifa ya kamati aliyoiunda kuhusu uvamizi katika kituo cha utangazaji cha Clouds.

Tulifanya mahojiano na wafanyakazi 14 wa kituo cha Clouds.-Balile

Tulifanya jitihada za kumtafuta Mkuu wa Mkoa, tulimpigia simu lakini hakupokea.- Balile

"Hata tulipofika katika ofisi yake, aliondoka kupitia mlango wa nyuma". -Balile

"Baada ya kushindwa kuonana naye, tukajiridhisha kuwa amechagua mwenyewe kutotumia fursa ya kuhojiwa". -Balile

"Katika uchunguzi wetu, tumejiridhisha kuwa Mkuu wa Mkoa alivamia kituo cha Clouds akiwa anaendesha gari mwenyewe". -Balile

"Kamati imejiridhisha kuwa RC na askari wenye silaha waliingia hadi ndani ya studio iliyokuwa ikirusha matangazo". -Balile

"Kamati imejiridhisha pia kuwa palikuwa na vitisho kwa walinzi na wafanyakazi kwa kutumia askari wenye silaha". -Balile

"Miongoni mwa vitisho ni kuwalazimisha kurusha kipindi vinginevyo angewaingiza kwenye tuhuma za dawa za kulevya". Balile

"Baada ya hapo aliwatisha kuwa yote yaliyotokea usiku ule, yabaki pale pale ndani" - Balile

"Tumejiridhisha kuwa RC Mkuu wa Mkoa aliingilia taratibu za uhariri kwa kulazimisha habari anayoitaka iruke" - Balile

"Kamati haikuona uthibitisho wowote kuwa kuna wafanyakazi waliopigwa na vitako vya bunduki au kupigwa mitama" - Balile

MAPENDEKEZO YA KAMATI

"Pendekezo la kwanza, Mkuu wa mkoa aombe radhi Clouds na kwa wanahabari wote" - Balile

"Pendekezo la pili, Waziri husika atoe taarifa kwa mamlaka husika ili Mkuu wa Mkoa achukuliwe hatua " - Balile

"Pendekezo la 3, ni vyombo vya usalama kufanya uchunguzi juu ya askari kuingia Clouds na silaha za moto" - Balil

Source: millardayo.com

Post a Comment: