Zoezi la uhakiki wa  utekelezaji wa masharti ya usajili wa Vyama va Siasa  kwa upande wa Tanzania Bara  linaendelea .Tayari  vyama 18 vimekwishakuhakikiwa. Vyama vinne vinatarajiwa  kuhakikiwa  Julai 4. Zoezi hili ni zoezi la kawaida na endelevu  ambalo hufanyika  kila mwaka ili kupima endapo vyama vya siasa   vinakidhi matakwa ya  Sheria ya usajili wa vyama vya Siasa.

Uhakiki wa Vyama vya siasa ni zoezi muhimu sana kwa sababu ni zoezi ambalo hugusa uhai wa  kila  chama cha siasa.  Kwa upande wa Tanzania Visiwani , uhakiki unatarajiwa kuanza  mara baada ya kumalizika Bara  kwa tarehe ambazo zitatangazwa baadaye.

Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Upande wa Usajili wa vyama vya Siasa , Bw. Sisty Nyahoza
Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Upande wa Usajili wa vyama vya Siasa , Bw. Sisty Nyahoza (kushoto) akihakiki daftari lenye orodha ya wanachama wa Chama cha NRA (National Reconstruction Alliance) wakati wa zoezi la kuhakiki wa utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa jana Jijini Dar es Salaam.
Msajili Msaidizi wa Vyama Siasa “Gharama za uchaguzi na Elimu kwa Umma “Bi. Piencia Kiurea (kushoto)
Msajili Msaidizi wa Vyama Siasa  “Gharama za uchaguzi na Elimu kwa Umma “Bi. Piencia Kiurea akimsikiliza Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha United Democratic Party (UDP) Bw. Godluck Ole-Medeye wakati akitoa taarifa muhimu za chama chake katika zoezi la Uhakiki wa Vyama vya Kisiasa unaoendelea Jijini Dar es Salaam.
Bi. Piencia Kiurea
Msajili Msaidizi wa Vyama Siasa  “Gharama za uchaguzi na Elimu kwa Umma “Bi. Piencia Kiurea akikagua baadhi ya taarifa za Chama cha Mapinduzi  “CCM” jana wakati wa  zoezi la uhakiki wa vyama vya siasa uliofanyika  katika  Ofisi  ndogo za  chama hicho  Jijini Dar es salaam.
Kaimu Mwenyekiti wa Chama Cha Democratic Party (DP) Bi. Georgia Mtikila
Kaimu Mwenyekiti wa Chama Cha Democratic Party (DP) Bi. Georgia Mtikila (kushoto) akitoa taarifa za chama chake kwa Afisa Sheria kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini (kulia), Bi. Jacqueline Kilama wakati wa zoezi la kuhakiki utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa Jijini Dar es Salaam Juni 28 mwaka huu.
Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Jahazi Asilia, Bw. Mbwana S. Kibanda
Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Jahazi Asilia, Bw. Mbwana S. Kibanda akifafanua jambo wakati wa zoezi la uhakiki  liliofanyika katika ofisi za chama hicho zilizopo ilala Jijini Dar es salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa chama hicho na kushoto ni watumishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
Bw.Eugene Kabendera, Katibu Mwenezi Taifa wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA)
Bw.Eugene Kabendera, Katibu Mwenezi Taifa wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) akitoa taarifa  wa watumishi  kutoka Ofisi ya Msajili wa vyama vya Siasa wakati wa Zoezi la uhakiki uliofanyika katika ofisi za chama hicho zilizopo Jijini Makumbusho Dar es salaam Jana.
Mhasibu kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw.Willium Brown Nyamtiga
Mhasibu kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Bw.Willium Brown Nyamtiga akisisitiza jambo kwa viongozi wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) Jana wakati wa Zoezi la uhakiki uliofanyika katika ofisi za chama hicho zilizopo Jijini  Buguruni Dar es salaam.
Bi. Esther Mwanri
Bi. Esther Mwanri, Mwanasheria kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa akikagua katiba ya Chama cha Wananchi (CUF) wakati wa Zoezi la uhakiki uliofanyika katika ofisi za chama hicho zilizopo  Buguruni Malapa Jijini Dar es salaam. Kushoto ni Bw. Shaweji Mketo, Mkurugenzi wa uchumi na Mipango.