WAKAZI WA KINONDONI KUANZA KUNUFAIKA NA UTAWALA WA CHADEMA
Wakazi wa mji wa
kinondoni,jijini D ar es salaam hivi karibuni wataanza kunufaika na utawala
mpya wa meya kutoka chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA ).Akiongea na
wananchi pamoja na waandishi wa habari hivi karibuni Meya huyo wa halmashauri
ya manispaa ya
kinondoni Mh Boniface Jacob , amesema “
mkakati wa kwanza walionao wao kama halmashauri chini ya utawala wake ni
kuwaondoa wakazi wa kinondoni katika dimbwi la hali duni ya maisha ilhali
kinondoni ndio wilaya inongoza kwa mapato Tanzania .katika kusapoti mkakati huo
wa halmashauri Mh BONIFACE JACOB ameanza kwa
kufuta bajeti ya viburudisho kwenye ofisi yake ya meya wa kinondoni badala
yake kuzielekeza pesa hizo huko kwenye ujenzi wa barabara mbalimbali zilizo
chini ya uangalizi wa halmashauri yake .
“inaumiza kuona
wananchi wako wakiangaika sehemu za biashara na kazi za kufanya halafu wewe
kama kiongozi unajiwekea bajeti ya mamilioni kwa ajili ya viburudisho ofisini !!”
mimi kama Boniface Jacob na
chama changu cha CHADEMA pia umoja wa UKAWA hatukubaliani na mfumo huo kandamizi.
Mh Boniface Jacob-Meya wa Kinondoni
Akifafanua zaidi Mheshimiwa meya amesema
Pamoja na hilo
halmashauri tayari imetenga kiasi cha pesa tsh bilioni 2.5 kwajili ya
kutengeneza vibanda vya matoroli ya kisasa kwa ajili ya biashara ndogondogo za
machinga ambavyo vitagaiwa kwa wananchi kwa ajili ya kuendesha maisha yao. Nia
na maudhui ni kuona kinondoni inazidi kusonga mbele kama halmashauri
inayojitegemea kwa mapato yake ya ndani wanaokusanya lakini pia wakazi wake wakishirikishwa
ipasavyo katika mchango wa kuendeleza wilaya yao.
“Manispaa ya kinondoni ina vyanzo 46 vya
mapato,na inaweza kukusanya mapato ya kiasi cha bilioni 46 ,ni wilaya tajiri
sana sema serikali ya CCM walikua wanaifuja hovyo”
Pia mh meya
amesisitiza kuwa tayari kuna mpango mkakati unaondelea baina ya halmashauri na
benki ya DCB ili kuwawezesha kina mama na vijana wa wilaya ua kinondoni kwa kuwakopesha mitaji midogo midogo na yenye
riba nafuu ili waende kuanzisha biashara mbalimbali .katika kuhakikisha hili
linafanikiwa halmashauri wameshatoa takribani milioni 200 kwenda kwenye benki
hiyo ya maendeleo ya mkoa wa Dar es salaam (DCB)
Post a Comment: