Tuesday, 23 February 2016



DR . ALLY MOHAMEDY SHEIN


VIJANA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametakiwa kujizatiti zaidi kulinda na kuendeleza Mapinduzi ya mwaka 1964 na Muungano uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu ndiyo hazina na rasilimali kubwa waliyoachiwa na viongozi na waasisi wa Taifa la Tanzania, Julius Nyerere na Abeid Amaan Karume.

Mwito huo umetolewa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein wakati alipozungumza na viongozi wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoa wa kichama wa Mjini Unguja ikiwa ni sehemu ya ziara ya kuangalia maendeleo ya jumuiya mbalimbali za chama hicho Visiwani.

Alibainisha kuyalinda na kuyadumisha Mapinduzi na Muungano ni kulinda na kuendeleza amani na utulivu nchini hivyo vijana hilo ndilo jukumu lao la msingi kama warithi wa taifa, na kusema chama kilichoonesha nia ya kuyadumisha mambo yote ya msingi yaliyoachwa na waasisi wetu ni Chama Cha Mapinduzi.

“Hakuna mbadala wa Mapinduzi, hakuna mbadala wa Muungano wala hakuna mbadala wa amani na utulivu wa nchi yetu hivyo ni lazima vijana mchukue nafasi yenu kulinda misingi hiyo ya nchi yetu kwani baadhi ya vyama vya siasa havina nia kama hiyo ya Chama Cha Mapinduzi cha kulinda urithi huo,” alisisitiza Dk Shein.

Alisema kazi kubwa iliyofanywa na waasisi hao wakati huo wakiwa vijana matunda yake yameonekana kwa hivyo aliwataka vijana wa sasa kufanya kazi kwa bidii na kuyaenzi mambo yote mazuri waliyoachiwa kwa faida ya kizazi kijacho katika kupiga hatua kubwa ya maendeleo na kupambana na umasikini.

SOURCE : http://mtembezi.com

Post a Comment: