MEMBE ASUTWA NA WASOMI WA CCM ....
KUSAFIRI NJE YA NCHI
Ndugu
Membe anapotosha ukweli anaposema Tanzania sio kisiwa na kwamba Raisi
na waziri wake wa mambo ya nje lazima wasafiri nje ya nchi watake
wasitake.
Tunapenda
kumfahamisha ndugu Membe kuwa, mh. Raisi Dr. John Magufuli hajatoa
kauli kuwa yeye au wasaidizi wake hawatosafiri nje ya nchi katika safari
za muhimu na zenye tija. Isipokuwa, muongozo wa mh. Rais kuhusu safari
za nje unalenga kupunguza safari zile ambazo hazina ulazima na tija kwa
taifa.
KUHUSU MGOGORO WA UCHAGUZI WA ZANZIBAR
Katika
maelezo aliyonukuliwa na gazeti la Mwananchi, ndugu Membe alieleza
kupinga kufutwa kwa matokeo yote ya uchaguzi wa Zanzibar yakiwemo ya
wawakilishi, na kwamba jambo hili limeihuzunisha dunia.
Kauli
hii ya ndugu Membe inatushangaza na kutusikitisha sana. Kwanza
tunajiuliza, Je, ikiwa sehemu kubwa ya uchaguzi iligubikwa na
udanganyifu na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi kinyume na sheria za
uchaguzi wa Zanzibar, ni kwanini ndugu Membe ashangae uchaguzi wote
kufutwa na tume ya uchaguzi ZEC?
Tunamtaka ndugu Membe atueleze, ni dunia ipi hiyo inayotushangaa?
Ni
kwanini dunia hiyo anayoitetea ndugu Membe haijashangaa kumuona maalim
Seif Shariff Hamad akijitangaza kuwa mshindi kinyume cha sheria za
uchaguzi?
Ndugu
Membe anapaswa kushangaa, ni kwanini hadi leo hii maalim Seif Shariff
Hamad hajakamatwa na kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya
kujitangaza kuwa mshindi kinyume cha sheria.
KUHUSU VIKAO VYA MARIDHIANO
Kuhusu
vikao vya maridhiano vilivyokua vinaendelea, ndugu Membe amekosoa
kitendo cha Raisi wa Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na maalim Seif
Shariff hamad kuachwa wakazungumza wenyewe wawili.
Kwanza
tunasikitika kuwa ndugu Membe huenda ama hajui kinachoendelea Zanzibar
au ameamua kupotosha umma kwa makusudi. Hii ni kwasababu mazungumzo
yaliyokua yakiendelea Zanzibar, hayakuwahusisha Dr. Shein na maalim Seif
Shariff peke yao. Bali yalishirikisha marais wastaafu wa Zanzibar,
Raisi wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, Makamu wa kwanza wa Rais wa
Zanzibar na makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar.
Pili,
katika muafaka wa kisiasa wa Zanzibar wa mwaka 2009/2010 uliopelekea
kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa, kwa kiasi kikubwa ni maalim
Seif Shariff hamad na Rais wa Zanzibar wa wakati huo mh. Amani Abeid
Karume pekee walioshiriki mazungumzo.
RAI KWA NDUGU MEMBE
Mosi,
tunapenda kumkumbusha ndugu Bernard Membe kuwa yeye ni mjumbe wa
Halmashauri Kuu ya CCM taifa amewahi kuwa mjumbe wa kamati kuu ya CCM.
Hivyo anajua utaratibu wa Chama na anayo nafasi ya kuyasema mawazo yake
juu ya uendeshaji wa serikali ndani ya vikao halali vya chama. Aidha,
ndugu Membe kwa nafasi yake kama mjumbe wa NEC na waziri wa zamaniwa
mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa, anayo nafasi ya kutoa ushauri
na maoni yake moja kwa moja kwa Raisi wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania mh. Dr. John Magufuli, Mwenyekiti wa CCM taifa Dr. Jakaya
Kikwete au kwa Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana.
Kutotumia fursa hizo kutoa maoni yake ni kujishushia heshima mbele ya jamii.
Pili,
tunamkumbusha ndugu Membe kuwa yeye sasa ni mstaafu aliyeitumikia nchi
yake kwa muda mrefu na nafasi mbalimbali. Ni vema sasa akatoa fursa kwa
viongozi wengine walioko madarakani kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia
watanzania. Muda wake umekwisha na sasa ni busara akakaa kimya na
kuchunga maneno yake.
Raisi mstaafu wa awamu ya tatu mh. Benjamin William Mkapa aliwahi kusema (nanukuu):-
"Siku
moja mtoto mdogo aliwahi kuniuliza. Nani ni bingwa wa kuendesha
shughuli za serikali? Nikatafakati sana swali lile, kisha baada ya muda
nikamjibu…Ni mwanasiasa aliyestaafu kisha akachunga ulimi wake…"
MWISHO
Tunamshauri
ndugu Membe kuuchukua ushauri huu wa Raisi mstaafu Benjamin Mkapa,
utamsaidia. Aidha tunamtaka afahamu kwamba watanzania wana imani kubwa
na juhudi zinazofanywa na serikali katika kupunguza matumizi, kuziba
mianya ya rushwa, ukwepaji kodi na ubadhirifu wa mali za umma. Wakati
huu si wa kupika majungu, fitina wala ubabaishaji. Ni wakati wa kuungana
pamoja kama taifa na kuchapa kazi tu.
Asanteni.
Imetolewa na ndugu
ALLY S. HAPI
KATIBU WA IDARA,
ELIMU, UTAFITI NA UONGOZI,
Post a Comment: