RAIS MAGUFULI AKUSUDIA KUUNDA MAHAKAMA YA RUSHWA NA UFISADI
…………………………………………………………….
Na: Immaculate Makilika, MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amezindua Bunge la 11 leo mjini Dodoma na kusema anakusudia kuunda Mahakama ya rushwa na ufisadi ili kusaidia kutatua kero hiyo ambayo imeonekana kukera wananchi wengi. Rais Magufuli amezindua Bunge hilo kwa mujibu wa Ibara ya 97, Ibara ndogo ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Rais Magufuli amesema, “wananchi wamekua wakilalamika sana juu ya rushwa na ufisadi unaondelea nchini kwa kusababisha wananchi kutopata haki zao na kutatuliwa shida zao kwa wakati, kati ya mambo ninayokusudia kuyashughulikia ni pamoja na kuunda Mahakama rushwa na mafisadi.” Kwa mujibu wa Rais Magufuli maeneo mengine ambayo wananchi wameyalalamikia ni pamoja na matatizo ya upatikanaji wa maji, migogoro ya ardhi, mgogoro ya mipaka kati ya vijiji na hifadhi za taifa, huduma za afya ,madini, kilimo, reli, elimu, ajira, haki za wazee, na maslahi ya wafanyakazi na wasanii. Pamoja na hayo Rais Magufuli amesema Serikali ya Awamu ya Tano itaondoa urasimu katika uwekezaji na kutowavumilia wale wote watakaokwamisha nia za wawekezaji wanaokuja kuwekeza nchini. Aidha, Dkt Magufuli ameeleza kuwa awamu hii ya Tano, itaweka msisitizo katika ujenzi wa viwanda ambavyo vitazalisha mahitaji ya watu (mass consumption) na kusema kuwa “waliobinafsishiwa viwanda waanzae kazi mara moja ,Serikali yangu haitawavumilia.” “Tutatatua kero za wananchi, na kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuimarisha Muungano. Muungano wetu ndio umoja wetu”. Kwa mujibu wa Rais huyo wa awamu ya Tano, yatakayoshughulikia ni pamoja na mchakato wa Katiba, Upanuzi wa barabara, reli na masuala ya uchumi. Rais Magufuli anakua Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu mwaka 1961 baada kuibuka mshindi kwa zaidi ya asilimia 50 dhidi ya mpinzani wake wa karibu Edward Lowassa katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 25 Oktoba , 2015.
Rais Magufuli azindua rasmi Bunge la 11 mjini dodoma
Kabla ya Rais Dkt. Magufuli
kuzindua Bunge, Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju aliomba Bunge
likubali kutenguliwa kwa kanuni za Bunge ili kuruhusu wageni kuingia
ndani ya Bunge hilo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe magufuli akihutubia Bunge la Jamhuri kama
ishara ya kuzindua Bunge la 11.
Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim
Majaliwa akitoa hotuba ya kuahirisha Bunge hadi mwezi Januari mwakani
baada ya Mhe. Rais kulizindua Bunge hilo.
Spika Job Ndugai akatoa amri ya
kuwataka wabunge hao kuwa watulivu na walipokaidi amri hiyo akatoa amri
ya kuwataka watoke nje ya ukumbu wa Bunge.
Baada ya Mwanasheria Mkuu kutoa hoja Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson akawahoji wabunge.
Mbunge wa Singida Mashariki Tundu
Lissu akiomba mwongozo wa Naibu Spika kwa kile alichodai kuwa kanuni
zimekiukwa.Hata hivyo, kiongozi huyo wa Bunge alitoa mwongozo na baadaye
alisitisha Bunge kuwaruhusu wageni kuingia kwenye ukumbi wa Bunge.
Baadhi ya wabunge wa upinzani wakiteta jambo wakati wageni wakiingia Bungeni.
Makamu wa Rais wa Tanzania Samia
Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
wakifuatilia yanayojiri Bungeni.
Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia
Ackson (kushoto), Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Jaji Othman Makungu, Jaji
Mkuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman na Spika wa Baraza la
Wawakilishi Pandu Ameir Kificho wakiingia kwenye ukumbi wa Bunge huku
wakiongozwa na mpambe wa Bunge.
Baada ya viongozi hao kuwasili
kwenye ukumbi wa Bunge, wabunge wa Upinzani waliendelea kupiga meza na
kuimba, hali iliyofanya ukumbi wa Bunge ukose utulivu.
Viongozi mbalimbali wakiwemo
Marais wastaafu, wakuu wa vikosi vya majeshi ya Ulinzi na Usalama,
Maspika wastaafu, Watendaji Wakuu wa Serikali, Mawaziri Wakuu wastaafu
na wageni wengine wakisikiliza hotuba ya Rais.
Baadhi ya wakuu wa mikoa, viongozi wa dini na wageni wengine waalikwa wakimsikiliza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Wabunge wote wa upinzani wakatoka
nje ya ukumbi wa Bunge isipokuwa Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT
Wazalende,Zitto Kabwe aliendelea kubaki ukumbini.
Wabunge walionesha kuridhishwa na hotuba ya Mhe. Rais Makufuli, wakipiga meza kuunga mkono hotuba hiyo.
Baada ya kukamilika kwa kazi hizo,
Mhe. Rais Magufuli akasindikizwa na wapambe wa Bunge kutoka nje ya
Bunge huku akiambatana na Spika wa Bunge Job Ndugai.
Baadhi ya Mabalozi na wawakilishi kutoka nchi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya Mhe. Rais Magufuli.
Mhe. Rais Dkt. Magufuli (wa pili
kushoto) akiwa na Marais Wastaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili
kulia), Benjamin Wiliam Mkapa (kulia) na Alhaj Ali Hassan Mwinyi
(kushoto).
Mhe. Rais Dkt. Magufuli (wa tatu
kulia) akiwa na Spika wa Bunge Job Ndugai, Makamu wa Rais Samia Suluhu
Hassan na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa (kulia kwake) na Rais wa
Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) na Marais Wastaafu Alhaj
Ali Hassan Mwinyi (kushoto) na Amani Abeid Karume (kulia).
Post a Comment: