Katibu UVCCM Wilaya Ateuliwa Kuwa Mbunge Viti Maalum Chadema

Katika
hali isiyotarajiwa na wengi, Katibu wa UVCCM wilaya ya Mbulu mkoani Manyara,
Bi. Anna Gideria ameteuliwa na Chadema kuwa mbunge wa viti maalum.
Bi.
Gideria amejiuzulu nafasi ya ukatibu na kukabidhi barua yake kwa mwenyekiti wa
UVCCM mkoa wa Manyara, Bi. Regina Ndege baada ya kutangazwa majina ya viti
maalum na jina lake kuwa katika orodha ya wabunge wa Chadema.
Akizungumzia
hatua hiyo, Bi. Ndege alieleza kuwa Bi. Gideria alipoteza imani na CCM muda
mfupi baada ya jina la waziri mkuu wa zamani, Frederick Sumaye kukatwa katika
kinyang’anyiro cha kumtafuta mgombea urais kwa tiketi ya CCM.
Mwenyekiti
huyo alieleza kuwa Bi. Gideria alikuwa ‘Team Sumaye’ na aliomba likizo ya mwezi
mmoja baada ya jina la waziri mkuu huyo wa zamani kukatwa.
“Baada
ya Sumaye kutoswa, alipoteza imani na CCM na ilipofika wakati wa kampeni mwezi
Agosti aliandika barua ya kuomba likizo na kukabidhi ofisini kwa mjumbe wa
kamati ya utekelezaji ya UVCCM wilaya ya Mbulu,” alisema Bi. Ndege.
Blog SiasaLeoTz lilijitahidi kumtafuta Bi Anna Gideria ili kujua sababu zilizosemwa na mwenyekiti wake wa zamani zina ukweli kiasi gani, na kumpata ambapo yeye binafsi amekiri kuwa
alipoteza imani na ccm tangu kwenye mchakato wa urais uliofanyika mwezi julai Dodoma, na si kwasababu mh Sumaye alikatwa ila ni kwakuwa mchakato
mzima ulikiuka taratibu za chama, na kuwepo ubabe wa hali ya juu kwa viongozi
wakubwa dhidi ya demokrasia. hivyo hakuona tena haja ya kuendelea kuwa
mwanachama na kiongozi wa chama kinachobaka demokrasia.
Post a Comment: