Sunday, 25 October 2015


JUMA HAJI DUNI - MGOMBE MWENZA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUPITIA CHAMA CHADEMA CHINI YA MWAMVULI WA UKAWA


Mwanasiasa machachari wa upinzani kutoka Zanzibar, Juma Duni Haji  mgombea mwenza wa mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Edward Lowassa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA); aliteuliwa kuwa mgombea mwenza mara tu baada ya mwanasiasa huyo kukihama Chama cha Wananchi (CUF) ikiwa ni sehemu ya makubaliano ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA - vyama vingine vilivyomo kwenye Ukawa ni NCCR-Mageuzi na National League for Democracy (NLD)).
Viongozi wa UKAWAwalipokutana kupitia majina ya wanasiasa wenye sifa ya kuwa wagombea wenza, walikubaliana kumteua mwanasiasa huyo ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF na Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) inayofanya kazi chini ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK).
Mwanasiasa huyo amekuwa na historia ndefu na mara tatu amewahi kuteuliwa na CUF kuwa mgombea mwenza wa urais wa Jamhuri ya Muungano, akiwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba. Amekuwa mgombea mwenza wa Profesa Lipumba katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1995, mwaka 2005 na mwaka 2010. Duni amewahi kunukuliwa akieleza kuwa yeye ni mtumishi wa watu na kila mara alikotumwa alikwenda. Hivyo, hata leo akiteuliwa kwenda kuongoza kijiji au kitongoji ilimradi Watanzania wametaka hivyo, ataitikia wito.

Juma Duni alianza safari ya kisiasa kwa “kulazimishwa” mwaka 1984, baada ya Serikali ya Muungano kutoa Waraka wa Serikali (White Paper) na kutakiwa wananchi watoe maoni yao juu ya hali na matatizo ya Muungano.
Wakati huo, makatibu wakuu wa Serikali ya Zanzibar akiwamo yeye walitoa maoni dhidi ya muungano. Uhuru huo wa kitaalamu uligeuzwa kuwa mchungu kwani walisingiziwa kwamba wamefanya kinyume na walivyoagizwa na baadhi yao wakapewa onyo kali na wengine wakateremshwa vyeo.
Juma Duni aliteremshwa cheo kutoka wadhifa wa Katibu Mkuu hadi mwalimu wa kawaida kwa Tangazo la Rais. Huko nako pia hakubaki salama kwani alituhumiwa kuwajaza wanafunzi kasumba, hivyo alirudishwa Wizara ya Elimu kama Ofisa Mipango ambako pia alituhumiwa kujihusisha na siasa za upinzani. Duni alipoona amechoka kuhamishwahamishwa na kushutumiwa, aliomba likizo ya bila malipo kwenda kusoma, ombi ambalo pia lilikataliwa.
Hapo ndipo alipoamua mwenyewe kuondoka na kwenda kujisomesha kwa fedha zake Chuo Kikuu cha Manchester, Uingereza na kuhitimu stashahada ya Juu ya Biashara kati ya mwaka 1993-1994. Alipofika Uingereza, akatumiwa barua ya kuachishwa kazi na kupoteza haki zake zote za miaka 18 ya utumishi serikalini.

Mwaka 1994 akiwa bado nchini Uingereza, akaunganisha masomo na kusomea 

Shahada ya Uzamili akibobea kwenye usimamizi wa Rasilimali Watu na kabla

hajahitimu akarejea nchini ili kusaidia upinzani kujipanga kiuchaguzi. Moja 

kwa moja akajiunga na vuguvugu la uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 

akajiunga na CUF na akateuliwa kuwa mgombea mwenza wa mgombea urais 

wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho, Profesa 

Lipumba wakati bado hajakamilisha shahada yake ya pili ya uongozi na utawala

Post a Comment: