TUJIKUMBUSHE : HUYU NDIYE EDWARD NGOYAI LOWASSA
Edward
Ngoyai Lowassa alizaliwa Agosti 26, 1953 na katika Kijiji Cha Ngarash huko
Monduli, Lowassa ni mtoto mkubwa wa kiume kwa mzee Ngoyai Lowassa.
Kielimu,
Lowassa ana Shahada ya Uzamivu (masters degree) katika Maendeleo kutoka Chuo
Kikuu Cha Bath nchini Uingereza aliyohitimu mwaka 1984, na kabla ya hapo
alihitimu shahada ya kwanza katika Chuo kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1977.
Kikazi,
Lowassa amekulia na kufanya kazi zaidi ndani ya CCM na serikali yake. Lowassa
amejiunga na CCM akiwa chuo kikuu cha Dar es Salaam. Huko alikuwa mwanachama
hai na baadae kiongozi wa Tanganyika African National Union (TANU) Youth League
(baadae CCM Youth League). Mara baada ya kuhitimu masomo, aliajiriwa na CCM
kama katibu msaidizi na baadaye katibu wa wilaya. Akiwa kijana ndani ya CCM
alipata kuwa msaidizi wa Mzee Rashid Mfaume Kawawa, Daudi Mwakawago na Horace
Kolimba.
Mzee
Kawawa alikuwa Waziri Mkuu wa Tanganyika na Tanzania, mmoja wa waasisi wa chama
na taifa letu. Bila shaka Lowassa alijifunza mengi kutoka kwake, na kama sio
utiifu wa hali ya juu na uzalendo wake kwa taifa, asingekweza kufanya kazi na
mzee Kawawa,anayesifika kuwa na misimamo ya hali ya juu.
Pia
Lowassa ni Luteni wa jeshi, licha ya kupigana vita dhidi ya Idd Amin nchini
Uganda mwaka 1978/1979, pia akiwa jeshini alifanya kazi kwa ukaribu na Rais
Jakaya Kikwete pamoja na katibu mkuu wa CCM wa sasa Mh Abdulrahman Kinana. Wote
tunajua kuwa jeshini ndiko kulikobobea kwa kufunzwa uzalendo na utiifu wa hali
ya juu.
Mwaka
1985,Lowassa aliteuliwa kuwa Mbunge kupitia Umoja Wa vijana CCM (UVCCM),
sambamba na Mama Anne Makinda (Spika wa Bunge la sasa) na Jenerali Ulimwengu.
Mwaka 1990 alichaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Monduli akipeperusha bendera ya
CCM ambako amekuwa mwakilishi hadi leo.
Toka
mwaka 1977 Lowassa amekuwa akiaminiwa na CCM na hakuwahi kukiangusha, amekwisha
kabidhiwa dhamana nyingi za uongozi zenye kumpa dhamana ya kusimamia na
kutekeleza ilani za chama, nyadhifa ambazo kila wakati alizitekeleza kwa
ufanisi wa hali ya juu. Lowassa amekwisha kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania
(2005-2008), Waziri wa Maji na Mifugo (2000-2005), Ardhi na Makazi (1993-1995), Haki na Mambo ya Bunge (1990-1993), na
Mazingira na Mapambano dhidi ya umasikini katika ofisi ya Makamu wa Rais.
mwaka
2008 alikubali kwa ridhaa yake kuachia nafasi yake ya Uwaziri Mkuu ili kulinda
heshima ya serikali nzima, Chama tawala CCM na pia ili kuepuka mgawanyiko
miongoni mwa wanachama, wananchi na viongozi. Huu ni uungwana na uzalendo wa
hali ya juu, wenye moja ya vielelezo vya utawala bora.
Mwaka
2014 tumeshuhudia sakata la Escrow ambapo pamoja na kuwa na ushahidi wa wazi wa
pesa kwenye akaunti zao, baadhi ya Mawaziri waligoma kuwajibika kwa hiari yao
na wengine kusimamishwa kazi na Rais. Lowassa alijiuzuru kwa tuhuma tu, ambazo
hazikuwa na mashiko wala ushahidi yakinifu, wala walau kupewa nafasi kuhojiwa
na kamati teule ya bunge.hivyo
nydhifa ya juu aliyowahi kushika ndani ya serikali ni waziri mkuu wa jamhuri
wa muungano wa
Tanzania ambapo Alichaguliwa rasmi kuwa
Waziri Mkuu wa
kumi wa Tanzania tarehe 30 Desemba 2005 akajiuzulu tarehe 7
Februari
2008 kwa kashifa ya Richmond. Sasa ni mgombea urais kupitia Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) chini y amwamvuli wa umoja wa
katiba ya
wananchi (UKAWA)
Post a Comment: