Saturday, 17 October 2015

Deo Filikunjombe aliyekuwa anatetea jimbo lake la LUDEWA kwa tiketi ya CCM anakuwa mbunge wa sita kupoteza maisha katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu na hivyo utalazimu pia uchaguzi wa ubunge kuahiriswa kwenye jimbo hilo.

Polisi katika eneo la ajali ya chopa ya Filikunjombe
                   Polisi katika eneo la ajali ya chopa ya Filikunjombe
Kamishna wa operesheni na mafunzo wa Jeshi la polisi, nchini Tanzania Paul Chagonja amethibitisha kutokea kwa ajali ya helikopta  Nnamba 5YDKK katika eneo la pori la selous kwenye kijiji cha Mtende mkoani Morogoro iliyosabaaisha vifo vya watu wanne akiwemo mgombea wa ubunge jimbo la Njombe Deo Filikunjombe.

Wakati Akizungumza na Sauti ya Amerika kwa njia ya simu jana tokea eneo la tukio kamishna Chagonja amesema maiti nyingine iliyotambulika ni ya rubani wa helikopta hiyo William Slaa  huku abiria wengine wawili ambao ni wanaume wakiwa bado hawajatambulika.

Filikunjombe ambaye alihitimu shahada ya uandishi katika chuo kikuu cha Makerere Uganda amewahi kufanya kazi katika vyombo vya habari nchini Tanzania kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa Njombe katika uchaguzi wa mwaka 2010.

Taarifa za kuanguka kwa helikopta iliyopoteza uhai wa Filikunjombe aliyekuwa mbunge machachari na makamu mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za serikali katika bunge lililopita zilianza kusambaa Alhamisi jioni katika mitandao mbalimbali ya kijamii na hatimaye majira ya mchana Ijumaa ndio ikathibitika kwamba watu wote waliokuwemo kwenye helikopta hiyo wamefariki dunia

Kamishna Chagonja amesema polisi na taasisi nyingine ikiwemo mamlaka ya usalama wa anga imeanza uchunguzi wa chanzo cha ajali hiyo ya helikopta ambayo inadaiwa ilikuwa imekodiwa na marehemu Deo Filikunjombe 
naye mwenyekiti wa kamati ya mazishi ambaye alikua ni mwenyekiti wa kamati za hesabu za serikali na rafiki wa marehemu Mh Zitto Zuberi Kabwe amesema tayari miili ya marehemu imeshafikishwa jijini Dar es salaam na kuhifadhiwa katika hospital ya rufaa ya jeshi lugalo na kwakuwa imeharibika sana mazishi yanatarajiwa kufanyika ndani siku mbili zijazo

Deo Filikunjombe anakuwa mbunge wa sita kupoteza maisha katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu na hivyo utalazimu pia uchaguzi wa ubunge kuahiriswa kwenye jimbo hilo.
na ufuatao ndio wasifu wa marehemu kwa mujibu wa ofisi za bunge   

GENERAL
SalutationHon.Member picture
First Name:Deo
Middle Name:Haule
Last Name:Filikunjombe
Member Type:Elected Member
Constituent:Ludewa
Political Party:Chama Cha Mapinduzi
Office Location:Box 12707, Dar Es Salaam
Office Phone:+255 752 087766/+255 774 776688Office Fax:
Office E-mail:dfilikunjombe@parliament.go.tz
Member Status:Active
Date of Birth4 March 1972
EDUCATION
School Name/LocationCourse/Degree/AwardStart DateEnd DateLevel
Ludewa Primary SchoolCPEE1986To DatePrimary School
Kasita Seminary Mahenge DioceseCSEE19891992Secondary School
Forest Hill Secondary School, MorogoroACSEE19941996Secondary School
Matola Pre-Form One Seminary, NjombeCSEE19881989Secondary School
CCP Moshi Police Training School, KilimanjaroCertificate (Basic Field Craft)20002001Certificate
Center For Foreign Relations College, Dar Es Salaam, TanzaniaLanguage Course20012002Certificate
Makerere University (MUK), Kampala - UgandaBA (Mass Communication)19961999Masters Degree
EMPLOYMENT HISTORY
Company NamePositionFromTo
The Parliament of TanzaniaMember - Ludewa Constituency20102015
World Vision International, TanzaniaCommunications Manager2005To Date
World Vision International, TanzaniaPublic Relations Communications Coordinator20022005
Public Exhibition, Benchmark ProductionResearch Assistant20022002
Tanzania General ElectionsMedia Monitor20002000
The New Vision NewspaperFreelance Photographer19981999
TAZAMA, Makerere University, UgandaCommunications Manager19981999
The Guardian Newspapers, Dar Es Salaam, TanzaniaColumnist19972002
Radio One Stereo, Kampala - UgandaCorrespondent19972001
National Television, ITVStringer19962001
POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/LocationPositionFromTo
Chama Cha Mapinduzi, CCMDistrict Youth Commander2009To Date
Chama Cha Mapinduzi, CCMSecretary (Ludewa District - Economics & Finance)2006To Date
Chama Cha Mapinduzi, CCMMember - Iringa Region Political Committee2006To Date
PUBLICATIONS
DescriptionDate
D. Filikunjombe: The Role of the Electronic Media in the Campaign against HIV/AIDS in Tanzania2010
                                                            

Post a Comment: