SENTENSI KADHAA KUTOKA VIONGOZI WA CHADEMA KATIKA MKUTANO NA WANDISHI HABARI LEO TAR 25/10/2015 JIJINI DAR ES SALAAM
PROF BAREGU MWESIGA
PROF
BAREGU : tumezoea swala kubwa katika
uchaguzi ni la amani na jambo libnalochangia ni wapiga kura kuoa wametendewa
haki.hivyo natoa tahadhari kwamba kama Watanzania watasoma matokeo hayajafanana
na watu walivyopiga kura zao HAWATAKUBALI. kisha kukawa na uwezekano mkubwa na watanzania kukataa
matokeo na kusema liwalo liwe.ni wazi tangu jana tumeanza kuona dalili la
uchaguzi huu kuharibiwa (rigging) kwa kukamta karatasi ambazo zimeshapigiwa
kura.Kama njombe walikamata gari limetiwa moto tume imesema ndio vilikua vifaa
hivyo ila vinakupa picha jinsi gani watanzania wanataka haki.Mvomero pia,hapa
Dar es Salaam yamekamatwa hii ni mwanzo tu.Na tunaendelea na kusikiliza,ila
nataka kuwaonyesha HATARI iliyoko mbele yetu.
PROF
BAREGU : Kuna simu za viongozi wetu
zimekua jammed,mimi kwahivyo inita tu kila dakika mbili,hivyo hivyo mwenyekiti
freeman mbowe,mrema nakadhalika.Simu zinaita ukipokea inazima .Unaona sasa
tumetoka katika uchaguzi tumeingia katika psychology war fare.wakati rais
alivyofungua kampeni alisema maadui zetu ni kuwapiga tu,sasa uadui umetoka
wapi? Uchaguzi ni ushindani.na kama mchezo unabadilika na kama taratibu
zinabadilika wanavyoweza kubadilisha ndivyo na sisi tunaweza kubadilisha.
Akiongea kwenye mkutano huo pia
Prof Safari amesema
PROF
SAFARI: Tangu Vituo vya Uchaguzi vilivyofunguliwa asubuhi kumetokea matatizo
kadha wa kadha.Matatizo haya tunmepigiwa simu na mengine kuona katika TV Kama tukio la buguruni ilikua
direct sio heresay na tumeona waliohusikaKama tunaamini karatasi za kupigia
kura zimekutwa mahali mbalimbali na kama inaaminika anaekana na hizi karatasi
ni tume ya uchaguzi.
Hii
inamaanisha kwanza karatasi zimeibwa au tume imeungana na ccm kuharibu uchaguzi.na
matukio yaliyotokea ni ushahidi tosha tume ya uchaguzi sio HURU na HAKI,ushindi wetu ni tsunami na
kuna maeneo ambayo ngome zetu bado matokeo hayajafika.
PROF
SAFARI : Nimepata taarifa kutoka katesh manyara kwamba
kuna vijana kutoka shule ya sekondari NANGWA ambako wamekataliwa na mwl.wao
mkuu amewakatalia kwenda kupiga kura.Amewaruhusu wanafunzi 20 pekee.sababu Tume
haikuwaandalia wanafunzi wa vyuo mfumo wa kupiga kura ambao walijiandikisha
vyuoni na kwa sasa wako majumbani.
PROF
SAFARI : Serikali imetenda hili
makusudi na hili la sekondari ni mwendelezo na linahusiana .ila Safari hii
kumekua na tatizo nchi nzima la vifaa mfano Kimara stop over na saranga hadi
jioni vifaa havikua vimefika.
PROF
SAFARI :Tume ya uchaguzi ilikua imetoa
maelezo kuwa vifaa hivyo vilipelekwa jana saa tisa usiku vikaharibiwa na hadi
muda huu hawajarekebisha. Bali Polisi wamepelekwa kule kudhibiti watu,wapiga
kura wanasubiri vifaa ila wameletewa mapolisi ili kuwaogopesha na sio vifaa.
PROF
SAFARI : Na hata pemba hili limetokea
hakukua na karatasi za rais na hata karatasi za kujumlisha matokeo yake.na Voter
Register kuna watu wengi wameenda hawakukuta majina yao kama
Tanga,Singida,Pemba na Dar.
Naye meneja wa kampeni wa chama cha demokrasia na
maendeleo ndg John mrema akiongea na waandishi mahali hapo amesema
JOHN
MREMA : Mkoa morogoro wametumia mihuri
ya mwaka 2010 na Tumesikia maeneo baadhi watu hawajapiga kura na tume imeahidi
kuongeza muda nakuna maeneo bado hakuna karatasi za kujumlisha
matokeo ya urais pia. Kuhusu suala la kuhesabu
kura haswa mkoani Tanga RC ametangaza kuwa kura zitahesabiwa halmashauri
tumesisitiza kuwa ni kinyume cha kampeni.
kwa maeneo ambayo tayari tumeshapata matokeo
yetu yanaridhisha sana.Tumejiandaa tunaendelea na mawasiliano na mawakala wetu
mpaka saa sita usiku tutakua tumekusanya kura 70%.Tutakwenda tume na matokeo
yetu yaliyokusanywa .
JOHN
MREMA :Tunawatahadharisha kuhusu vituo
vyao vya Chang’ombe,oysterbay na kurasini tunapata taarifa ya michezo
wanayofanya na bahati nzuri wako wanaopenda mabadiliko katika vituo hivyo.maana
waliopiga kura sio polisi na jeshi ni wananchi na wameamua
Post a Comment: