Maalim Seif Sharif Hamad Atangazia umma Ushindi wa Urais Zanzibar..
Mgombea
urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad,
ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya chama
chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka vituoni, yeye amepata kura
200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa CCM anayetetea nafasi yake,
Dk. Ali Mohammed Shein.
Aidha,
akiongea na wanahabari, Maalim Seif Sharif Hamad ameitaka Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo halisi kama yalivyo kwenye
fomu zinazotoka vituoni.
Chanzo: DW
#ZanzibarYaamua2015.
Muda mfupi uliopita, mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF,
Maalim Seif Sharif Hamad, ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na
kusema kuwa baada ya chama chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka
vituoni, yeye amepata kura 200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa
CCM anayetetea nafasi yake, Dk. Ali Mohammed Shein, na kuitaka Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo halisi kama yalivyo kwenye
fomu zinazotoka vituoni. Mengi zaidi, sikiliza matangazo yetu ya leo
mchana.


Post a Comment: