KUTOKA MAGAZETINI LEO TAREHE 15/10/2015
Wapiga kura Tanzania watakiwa kujua utaratibu
Tume ya uchaguzi nchini Tanzania imewataka wananchi kujielimisha kuhusu utaratibu na haki yao ya kupiga kura kwa njia ya amani wakati wa uchaguzi mkuu Oktoba 25. Maafisa wa tume wanasema kwa wiki kadha sasa wamekuwa wakitoa elimu kwa wapiga kura kuhusu kile wanachotakiwa kufanya kuhakikisha hawapotezi haki yao ya kupiga kura siku hiyo itakapofika. Watanzania wapatao millioni 22 wanatazamiwa kushiriki katika zoezi hilo. Tume ya uchaguzi pamoja na makundi ya kijamii yanatoa maelekezo.....Published By: VOA News Swahili
Maalim Seif: Hakuna wa kuzuia mabadiliko Oktoba 25
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF chini ya mwamvuli wa Ukawa, Maalim Seif Sharif Hamad amesema hakuna wa kuyazuiya mabadiliko yajayo kupitia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu....
Maalim Seif kuzindua mpango wa kuifanya Zanzibar kuwa Singapore ya Afrika Mashariki
Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akiwahutubia wafuasi wa chama hicho katika viwanja vya jimbo la Mkwajuni. Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akikabidhi kadi kwa mmoja kati ya vijana 39 wa CCM jimbo la Mkwajuni waliojiunga na CUF Mwenyekiti wa Timu ya ushindi wa CUF Nassor Ahmed Mazrui, akiwahutubia wafuasi wa Chama hicho katika viwanja vya Mkwajuni. Wafuasi na wapenzi wa CUF wakifuatilia mkutano huo. Wafuasi na wapenzi wa CUF wakifuatilia mkutano huo.Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa timu...
Published By: ZanziNews
Rais Kikwete aonya wanaopanga kulinda kura vituoni
Rais Jakaya Kikwete amesema watu wanaopanga kubaki katika vituo vya kupigia kura baada ya kumaliza zoezi hilo kwa lengo la kulinda kura kunaashiria uvunjaji amani, hivyo serikali imejipanga kupambana na hali hiyo siku ya uchaguzi...
.Published By: Mwananchi
Post a Comment: