HEKAYA ZA MTAA : MWIZI HATUMWI WALA HAAMINIKI
Naam waungwana ,habari za juma ya wiki
!? vip huko mtaani kwenu ile habari ya mvua za elnino imeshaanza kujionyesha
ama la !? huku kwetu katika mtaa wa siasa kama ni elnino,basi elnino yetu
ilikua ni msiba wa wanaharakati wa mtaa.
Msiba wa kwanza ni wa Yule Ndg Kingunge nguli
wa harakati za uzalendo kwa miaka zaidi ya 61 alipokikimbia chama alichokijenga
na kukilea kwa miaka yote ya maisha yake sababu kimepoteza muelekeo na sifa za
kuongoza taifa,na yeye binafsi kutangaza
rasmi kusapoti ule upande wa wananchi wanaohitaji mabadiliko.hivyo basi uamuzi
wake umeacha na kupeleka kilio cha msiba kwa wale ndugu wana familia ya kijani
Huu msiba wa pili hakika umenitia
simanzi kubwa sana mwana hekaya sababu ,ndugu yangu huyu alikua jasiri,shujaa
na mwanaharakati wa kweli aliyesimama katika kila alichokiamini yeye siku zote
na mungu ailaze mahali pepa peponi roho yake mchungaji Christopher
Mtikila.AMINA
Pamoja na elnino hiyo kubwa haikuzia
kwenye baraza la mtaa kupata mawazo mapya na yakinifu kutoka kwa wana
jumuiya.na leo hacha mie niliwakilishe hili lilozua tafrani
Hakika katika jamii yoyote ile duniani
jamaa akishaonekana mwizi,mlafi na si muaminifu huwa hatumwi wala kuagizwa
jambo lolote kubwa lenye thamani na kuhitaji uaminifu.
Sasa wale ndugu wana jumuiya wa upande
wa pili wanapokaa na kusema eti huyu wa upande huu ni mwizi hafai kuaminika je wamefanya tafiti
yakinifu kweli !?
Maana wanapenda sana kumsingizia baba
yetu mkuu,ambaye udaktari wake kifalsafa hakumuondoa kwenye hadhi yake ya
ualimu lakini wanasahau kuwa ni huyu huyu ndie aliyemtuma kijana huyo
akamchukulie tunzo zake za heshima.enzi akiwa katibu mkuu msaidizi wa chama
tena hebu tazama yupo waziri wa mambo ya nje ambaye sisemi mengi juu yake
lakini mwalimu akamuamini katibu huyo wa chama.
TIZAMA PICHA HII
Halafu ndugu zangu mbona mmesahau kua
huyu mwenzetu anaaminika zaidi kuliko huyu mnayemuona mchapakazi na ndio maana
mwenyekiti wenu aliamua kumpa utendaji mkuu wa serikali ili aweze hata
kumuongoza huyo mnayesema mchapakazi!?
Tulikua na waziri ambaye huhusika ma
masuala ya nje na ushirikiano wa kimataifa ambapo kwa miaka 10 wa utawala wa Yule
kipara ambaye mnamheshimu sana japo ni bingwa matusi na sasa naye ni mkuu wa
kaya .hakuaminika hata chembe mbele ya kipara kwenda kuchukua ama kumuwakilisha
kwenye tafrija kubwa zilizohitaji mtu makini zaidi ya kua ni waziri wa kwenda
UN kushangaa wanamuziki lakini
akamuamini waziri wake wa maji kwenda kuwakilisha kwenye suala linalohusu
ushirikiano wa kimataifa na mikataba ya kitaifa na mwisho akamletea ushindi kwa wananchi wake na leo wanafurahia matunda hayo kwa kunywa maji safi.hakuishia hapo
alimpa uenyekiti wa kamati kwenda kufanya tafiti kwa nchi za wenzetu ni jinsi
gani twaweza piga hatua.kumbuka yupo waziri wa mambo ya nje na ushirikiano na
maagizo yanapita tu mbele yake
Naomba nihitimishe tu kwa kusema kama viongozi
watatu wa taifa hili kati ya wanne waliweza muamini na kumtuma kwanini wewe
usimuamini akakuongoza!?na unakaa kumuita mwizi pasipo shahidi pia ilhali wajua fika mwizi haaminiki na hatumiki.
ASUBUHI NJEMA
Post a Comment: