Monday, 12 October 2015


“Asamehewe Yule aliyejua maana ya msamaha na akamaanisha toka moyoni wakati akiomba msamaha” haya wahenga huita maneno ya busara lakini yenye haki ndani yake.inatupasa kukumbushana misemo kama hii hasa kipindi hiki tunachoelekea cha uchaguzi mkuu wan chi yetu ilhali tukiwa tumebakiza wiki mbili tu.Na wahanga wakubwa ni sisi wakazi wa mtaa huu wa siasa 

Mwisho wa wiki huu na matukio mengi na yenye kuteka sana hisia hasa wana familia kwakua muda mwingi tunashinda na familia zetu na kujua matatizo yanayotukabili.nikiwa  na vijana wangu tukipata pilau la mchana wa jumapili ndipo waliponiuliza swali hili “mbona mzee wa push up hajaonekana mtaani siku ya pili leo ??” kwanza walinishtua maana sikuzani kama vijana wangu watakua makini namna hiyo lakini pia sikua na jibu kamilifu la swali lao,hivyo nikawaomba niwasiliane na wajomba zao ambao tumeoleana ndoa ya kudumu katika familia mabadiliko ila wao ni wazaliwa wa familia ya mkwere.

Nilioyapata kuyajua huko ndio yamenifanya nione umuhimu wa kuwashilikisha vyema,ndugu zangu ule msemo wa wahenga usipime kwa macho kumbe una maana nzito hivyo.eti Yule bwana pamoja na mbwembwe zote zile za push up,kuruka kwenye gari,kukimbia stejini na kucheza mziki wa yamoto kumbe ni mzee wa mbio fupi marathon haziwezi !? sasa nikawa najiuliza hawa wenzie ambao kila siku wanashinda majukwaani kumpamba mara oooh huyu Usain Bolt mara oooh huyu miraba mine hakuna kitakachomshinda kumbe hawajui mwenzao ni mzee wa mbio fupi ? ona sasa wamemkimbiza tu nusu marathon anahemea juu juu siku mbili zote hizi haonekani.wakati Yule waliomdharau na kumdhihaki sasa ndio mwendo mdundo anaongoza marathon kwa mbwembwe zote. 

ILA YOTE KHERI KAMA YU MZIMA NA NAMUOMBA KUMPA USHAURI WA BURE HAYA MAMBO SIKU NYINGINE USIPIME KWA MACHO
  
                                                                                                                  

Post a Comment: