HEKAYA ZA MTAA: HODI HODI MAGOGONI NINA SALAMU ZA LUBUVA
Asaalamu waungwana, naona kumekucha tena
na zimebaki siku 23 kumjua mrithi wa mkwere.
Leo sitokua na nakuu kutoka mtaani maana
wamenipa salamu za jaji lubuva nizipeleke magogoni.
Ndugu mkuu wa kaya, vijana wako
wameniagiza wanaomba uwakumbuke wao sana sana pale mtakapokaa na jamaa zako wa
NEC kumpitisha rais ajaye baada yako maana wanaipenda Tanzania na hawataki
kukupeleka ICC
Lakini pia mkuu vijana wanaomba sanasana
yale magari yako yenye maji ya washa washa yasizunguke mtaani kutusumbua na
kutuonea bali mapema kabisa uwatafute hao mliowapa kadi za NEC zisizo halali.
Mh sana mkuu wa kaya .jamii ya mtaa wa
siasa inaomba upokee hizi salamu za jaji lubuva na umwambie sheria ni msumeno
hivyo kama lema aliwekwa ndani kwa kuzidisha dk 6 basi angalau hata kwa dakika
kadhaa muweke ndani magufuli na wenzie kwa kuwa ni mabingwa wa kuzidisha muda.
Lakini pia aache mara moja kuwa msemaji
wa chama cha mapinduzi ilhali veye sio nape bali yeye ni refa wa huu mchezo na
atumie sheria zote 17 za mchezo kuchezesha,masuala ya kesi kuletwa kwake (mfano
kesi ya bulembo ) na kutoa hoja nyepesi nyepesi katika majibu si sahihi.
Post a Comment: