HEKAYA ZA MTAA: JENERALI DAVIES MWAMUNYANGE KUWASILI LEO
Habari
wapendwa
Katika
hekaya za leo,mzee wa hekaya amedokezwa kuwa Yule mkuu wa majeshi ya ulinzi na
usalama nchini Tanzania,Jenerali Davies Adolph Mwamunyange atawasili leo kutoka ughaibuni.
Taarifa
za awali zilionyesha kuwa mkuu huyo ambaye ameleta taharuki kubwa wananchi kwa
wiki kadha sasa baada ya kusemekana yu mahatuti baada ya kunywa kitu
kinachodhaniwa ni sumu.angewasili nchini leo saa saba mchana,lakini zikaja
taarifa zaidi atawasili masaa mawili baadaye.
Na hadi mnyetishaji huyo akimpa habari mkuu wa hekaya za mtaa ni kwamba Jen Mwamunyange alikua hajawasili nchini ila kwa habari za ndani zaidi alikua
mahali kusubiri mapokezi ya kuingia nchini kwa utaratibu ambao jeshi letu la ulinzi na
usalama wenyewe wanaona unafaa kuandaliwa
Ikumbuke
kuwa taifa kwa ujumla liko katika shauku kubwa ya kumshuhudia kamanda wetu huyo
akijitokedha hadharani baada ya kuwepo tetesi za kua ni mgonjwa na wengine
kufika mbali na kudai tayari alishaaga dunia.habari ambazo zilichombezwa na
kukamatwa kwa mwanafunzi anayesadikiak kua ndio muanzilishi wa habari za
kudhuliwa na sumu kwa mkuu wa majeshi huyo.lakini taarifa hizi zimechukua
taswira mpya ya kisiasa zilizochagizwa na uchaguzi mkuu wa rais,wabunge na
madiwani. kiasi ambacho upo upande unaamini kuwa kamanda huyu mkuu wa majeshi
Tanzania ni kweli amenyweshwa sumu katika minijali ya kumdhuru baada ya
kuonesha msimamo wake nje ya ule wa serikali na ndio sababu iliompelekea kwenda
nje ya nchi kwa matibabu zaidi,lakini pia serikali na familia vikisisitiza kuwa
kamanda huyo yuko mzima salama salmin na yuko nje ya nchi kwa kazi maalumu
aliogizwa na rais na serikali.
Kwa kipindi
chote hicho haya yakiendelea jeshi letu la ulinzi na usalama kupitia msemaji
wake mkuu na idara ya habari ya jeshi hilo hawajatoa kauli yoyote ile,hali
ambayo imezidisha utata na kuwaweka wananchi njia panda ya nini kile haswa kinachoendelea
!?
Mzee
wa hekaya za mtaa yeye anaomba arudi
tu salama hii leo tumuone na azungumze nasi ili wananchi tuwe na amani moyo na
yeye aweze endelea kutulindia mipaka na usalama wan chi yetu mama pendwa
TANZANIA ila na kama yupo mtu alijaribu kumtenganisha kamanda wetu na sisi basi
ashughulikiwe ipasavyo.


Post a Comment: