HASARA YA UCHUMI INAYOSABABISHWA NA FOLENI
Report
za wachumi zinasema tanzania inapoteza bilion 4 kila siku kutokana na foleni
(shilingi bilion 4) hebu fikiria hii pesa inayopotea ingesaidia nini kwenye
uchumi wetu ingejenga madawati wangapi,zahanati ngapi kila siku.lakini jiji
linaloongoza kwa msongamano dar es salaam halmashauri za hili jiji zimepiga
kimya kila siku hela ziendelee kupotea
sasa
hivi nyumba nyingi za dar za kima cha kati kwenda cha juu kuna magari 4 uani
yamepakiwa asubuhi baba,mama watoto wote watatoka na magari kuelekea sehemu
hizi kariakoo,posta ndo kwenye maofisi mengi.ina maana kwa siku maeneo haya
makubwa ya mjini yanapatwa na magari madogo sio chini ya laki 2 yanaingia mjini
hii inaleta msongamano wengi wanatoka na magari binafisi sababu magari ya
public hayaaminiki usafiri sio salama.
maono
yangu kusaidia kupunguza foleni na kuokoa haya mabilioni kumbuka kwa mwaka ni
zaidi ya trilioni 1.4 tsh
1.kuboresha
usafiri wa mabus kuwe na mabus ambayo ni ya quality level seat kupeleka watu
makazini na kurudisha jioni
2.ikiwa
watu wataendelea kutoka na gari ndogo zijengwe sehemu mahalumu tuseme wakazi wa
mbezi ya kimara,kibaha wawe na sehemu ya kupaki magari ubungo kama utavuka
zaidi ya ubungo utalipia 5000 kwa siku kuingiza gari lako mjini
3.zijenge
reli kuanzia maeneo haya kibaha-posta,tegeta(bunju)-posta,mbagala-posta hii
itamaliza msongamano watu wengi watapanda treni na kuacha magari madogo
nyumbani
4.kuhamisha
malori yasipite mjini tena hii itakua na plan kubwa kuiendeleza kisarawe kwa
kujengwa bandari ya nchi kavu na kuboresha barabara ambayo itatokea hadi maili
moja hapa pia tutatanua mji wa kisarawe kuanzia barabara,ajira za kwenye
migahawa ambayo itafungiliwa njiani.hili lilitokea siku moja roli lilipata
ajali maeneo ya kibamba tulitumia masaa 6 kwenye foleni ndo unafika
nyumbani.zile bandari zote za nchi kavu zitaamia kisarawe mzigo baada ya
kupakuliwa bandarini utabebwa moja kwa moja kwenye bandari ya nchi kavu hapo
malori yatakuja na kupakia.
Sijaona
bado mradi wa mabasi ya mwendo kasi utapunguza vipi foleni sijaona bado.
faida
ya kufanya haya.
1.halmashauri
za wilaya zote ilala,kinondoni,temeke kuongeza mapato kutokana na makusanyo ya
parking za magari tozo la kuingia mjini na gari yako binafsi.
2.kuhifadhi
hizo bilioni 4 zinazopotea na kuongeza na bilioni 6 nyingine za kukusanya
mapato kama foleni itapungua na kuisha ina maana tunaweza tengeneza bilioni 10
kwa siku kwa mwaka ikapatika zaidi na trilioni 3.6 hebu jiulize pesa kama hiyo
ingesambaza maji kwenye jiji la daresalaam,ingejenga barabara ngapi tanzania
kwa mwaka,shule zahanati.
3.kupanua
wigo wa ajira kwenye treni,kwenye bandari ya nchi kavu kisarawe njia mpya ya
malori mashell yatajengwa,mahotel zoe ajira hizo.
mwisho
nashangaa baadhi ya watanzania ambao walishangilia mapinduzi ya burundi jana
ambayo hajafanikiwa kuchafuka kwa burundi kuatuathiri sisi kiuchumi mpaka sasa
tumepokea wakimbizi 17000 kigoma hawa wakimbizi wataharibu mazingira ya kukata
miti ili kuweka makizi.
lakini
pia inakua ni ngumu kufanya kazi na mtu ambaye anapigana mipaka ilifungwa jana
burundi tunajua nchi ambayo haina bandari inategemea vitu vingi kutoka kwetu
kutokuwa kwao salama ina maana ni ngumu kufanya biashara kama gari ya mzigo
ilikua uiende burundi haitakwenda.
Post a Comment: