Saturday, 3 October 2015

Wagombea wa vyama vikuu vinavyowania Ikulu ya Taifa vimeibeba juu kwa juu kauli mbiu ya mabadiliko huku upande mmoja ukishindwa kuainisha mkakati dhahiri wa kuyafanikisha mabadiliko hayo na pia bila kuyafafanua ni mabadiliko ya aina gani. Nionavyo kibinafsi kwa upande wa sisiem wanajaribu kutuaminisha kuwa mkakati wao unaitwa Magufuli. kuwa Mikopo ya wanafunzi, tusubiri Mgufuli aingie; madawa hospitalini, tusubiri Magufuli aingie; uonevu mama ntilie na machinga, tusubiri Magufuli aingie; uonevu na kubambikia kesi, tusubiri Magufuli aingie. hivyo wanataka tuaminisha Magufuli amekuwa ilani, sheria na katiba ya nchi. Mimi naona kama hiki ni kichekesho; sioni ni kwa vipi mwanadamu anavyoweza kuwa mkakati mahususi wa kumaliza matatizo ya Taifa zima; ni kwa vipi ataweza kuwepo kila mahali kwa wakati wote; na pia huyu ni binadamu anaweza kuugua au kupatwa na jambo lolote sijui hapo tunaenda wapi tena. Mkakati ni mbinu inayokaa kimaandishi na inayokuwa na nguvu zote za kisheria kuadabisha na kuwajibisha na wala si kwa kutumia akili ya mtu mmoja na kutegemea leo kaamkaje. 
Kwa upande wa upinzani mkakati wao ni maadili na ulinzi wa rasilimali za nchi unaoasisiwa na katiba ya wananchi, ingawa nao hawaonekani kuwa na ujasiri kamili wa kulisimamia hili waziwazi na hivyo kutuacha kidogo naswali hivi mabadiliko tunayoyasikia yanatofautiana au yanafanana. 
 Labda wao wanamaanisha mabadiliko kwa maana ya kuhama chama cha siasa au kuiondoa sisiem madarakani na kuleta hali bora zaidi za kimaisha; lakini yote haya yanawezekana kwao bila hata kuweka hadharani mikakati mahususi ya kuliwezesha hilo kwasababu  dhamira yao inajulikana ni nguvu ya umma.
 tofauti na ccm ilioamua kuwachanganya wapiga kura ili wajionea kwamba wote  upinzani na ccm  ndio walewale wala hamna tofauti na huenda hamna jipya ni porojo tu zilizozoeleka ili kupunguza imani ya jamii kwa ukawa.

Post a Comment: