BREAKING NEWZ : POLISI WAZUIA MKUTANO WA MAMA REGINA LOWASSA NA BAWACHA MLIMANI CITY
habari
zilizotufikia hivi sasa kutoka kwenye vyanzo vyetu vya habari ni kua jeshi la
polisi kanda maalumu ya Dar es salaam wamezuia mkutano wa Mke wa mgombea urais
kupitia CHADEMA,Mama Regina Lowassa
pamoja na baraza la wanawake chadema (BAWACHA) Ambao ulipaswa kuanza na matembezi ya amani kuliombea taifa amani.
Akiongea
na blog ya siasaleotz msemaji huyu
anasema mkutano huo ulikua halali na walipewa kibali cha kuufanya siku ya leo
lakini ghafla leo asubuhi kamanda mkuu wa kanda ya dar es salaam ,Kamanda Kova
alifikia mahali hapo akiwa na vijana wake
na kutoa amri ya kuzuia mkutano huo pasipo kua na maelezo ya kutosha
zaidi.hali iliopelekea kutoeleweka hivyo kuleta mabishano na baadhi ya wajumbe
wa BAWACHA hivyo kuwakamata akiwemo mwenyekiti wa baraza hilo.hadi habari hizi zinaenda hewani wajumbe hao
walikua bado hawajaachiliwa na polisi.
Post a Comment: