Saturday, 26 September 2015

Magufuli: Watanzania tusidekezwe na utafiti

*Asema hawezi kuwa rais bila kupigiwa kura *Aanza kurusha makombora Ukawa Na Bakari Kimwanga, Kahama MGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amewataka Watanzania kutodekezwa na matokeo ya utafiti unaoendelea kutolewa na taasisi mbalimbali.   Kauli hiyo aliitoa jana kwa nyakati tofauti, alipohutubia mikutano ya kampeni iliyofanyika katika majimbo ya Busanda, Mbogwe ya mkoani Geita na majimbo ya Ushetu na Kahama Mjini ya mkoani Shinyanga.   Alisema katu utafiti huo hauwezi kumfanya awe rais na hivyo ni lazima wana CCM na Watanzania kwa ujumla wampigie...
Published By: Mtanzania

Lowassa kidedea

*Aongoza kwa asilimia 54.5 *Asema Serikali dhaifu imesababisha migogoro   NA AZIZA MASOUD, DAR ES SALAAM   UTAFITI mpya uliofanywa na Taasisi ya Tanzania Development Initiative (TADIP) umeonyesha mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa, angeshinda kwa asilimia 54.5 kama Uchaguzi Mkuu ungefanyika ndani ya wiki tatu za Septemba mwaka huu huku mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli, angepata asilimia 40.   Matokeo ya utafiti huo yametolewa ikiwa ni siku chache baada ya wiki hii Taasisi ya Twaweza kutoa matokeo ya utafiti wao yaliyoonyesha kama kura zingepigwa Agosti na Septemba,...
Published By: Mtanzania 

Mgombea urais ampa ushindi Lowassa

Mgombea urais Chama cha Tanzania Labour (TLP), Macmillan Lyimo amepingana na matokeo ya tafiti za kisiasa yaliyotongazwa hivi karibuni na taasisi mbili, akisema kama Uchaguzi Mkuu ungefanyika Septemba, mgombea urais wa Chadema na Ukawa, Edward Lowassa ndiye angeshinda kwa kishindo....
Published By: Mwananchi

MAMBO MUHIMU AMBAYO LAZIMA UYAJUE KABLA YA MECHI YA SIMBA VS YANGA

Leo ni siku ambayo ilikuwa ikisubiriwa sana na mashabiki wengi wa soka la Tanzania, leo ndio siku ambayo unapigwa mtanange wa Dar es Salaam Darby (Yanga vs Simba) mechi hii inatajwa kuwa miongoni mwa Derby kubwa barani Afrika lakini ikiwa ni Derby yenye upinzani mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki. Simba na Yanga zinakutana leo kwenye raundi ya nne ya VPL lakini ikiwa ni mechi ya kwanza inayozikutanisha timu hizo msimu huu, hapa chini nimekuwekea vitu muhimu unavyotakiwa kuvijua kabla ya mechi haijapigwa ili wakati wa mchezo utapofika unakuwa unajua...
Published By: Shaffih Dauda

Gharika ya Lowassa ndani ya mji wa Mererani, Simanjiro Mkoani Manyara jana

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi wa Mji wa Mererani, katika Mkutano wa Kampeni zake, uliofanyika kwenye uwanja wa Machinjioni, Simanjiro Mkoani Manyara leo Septemba 25, 2015.Sehemu ya Wananchi wa Mji wa Mererani, Jimbo la Simanjiro Mkoani Manyara wakionyesha furaha yao mbele ya Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, wakati akiwahutubia katika Mkutano wa Kampeni zake, uliofanyika kwenye uwanja wa Machinjioni, Mererani, leo Septemba 25, 2015.Waziri Mkuu wa...
Published By: ZanziNews

Post a Comment: