KUTOKA MAGAZETINI LEO TAREHE 27/9/2015
Simanzi zatawala mapokezi mwili wa Celina Kombani
Huzuni, simanzi na majonzi jana vilitawala Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), wakati mwili wa Celina Kombani, aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, ulipowasili....Published By: MwananchiWapambe wanogesha kampeni Lowassa, Magufuli
Wakati wagombea urais wa vyama vya CCM na Chadema wakijikita kwenye
ahadi za mambo watakayofanya iwapo watachaguliwa, wapambe wao
wameendelea kufanya kazi ya kujibu kutuma mashambulizi kwenye kampeni
kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu zinazoendelea kote nchini....
Published By: Mwananchi
Lubuva: Uchaguzi huru na haki si jukumu la NEC pekee
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Damian
Lubuva amesema uchaguzi kuwa huru na haki, siyo jukumu la NEC pekee,
bali wadau mbalimbali....
Published By: Mwananchi
Magufuli awasha moto Shinyanga
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia
wakazi wa Shinyanga mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa
kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Kambarage ambapo aliwaambia
wananchi hao kuwa wakati umefika wa kujenga Tanzania mpya yenye viwanda
vya kutosha kutoa ajira kwa vijana wengi.Alisema pia kuwa Serikali yake
itakuwa rafiki wa sekta binafsi na kuwajengea uwezo wafanya biashara
ndogo ndogo ili waweze kujiendeleza. Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.
John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa Shinyanga kwenye mkutano wake
wa Kampeni ambapo aliwaambai wananchi hao kuwa serikali yake itakuwa...
Published By: ZanziNewsLowassa alipotinga jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akipokelewa na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Mh. Freeman Mbowe, wakati alipowasili eneo la Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Mpira wa Machame, Jimbo la Hai, Mkoani Kilimanjaro Septemba 26, 2015.PICHA NA OTHMAN MICHUZI.Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akimnadi kwa wananchi, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Hai na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia...Published By: ZanziNews
Post a Comment: