Tuesday, 29 September 2015

Nape atumia muda wa kampeni kutukana

Nape atumia muda wa kampeni kutukana Jonas Mushi na Veronica Romwald, Dar es Salaam MJUMBE wa Kamati ya Ushindi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye ametumia muda wote aliopewa kumnadi mgombeaa urais wa chama hicho, Dk. John Magufuli kumtukana mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anayewakilisha Ukawa, Edward Lowassa pamoja na viongozi wenzake. Katika mkutano huo uliofanyika jana katika viwanja vya Samora mjini Iringa na kurushwa moja kwa moja katika Kituo cha Star TV, Nape alitumia muda wake wote kumtukana Lowassa pamoja na viongozi wa Chadema...
Published By: Mtanzania

Lowassa apata mapokezi makubwa jimbo la Bumbuli mkoani Tanga

Wananchi wa Mji wa Soni katika Jimbo la Bumbuli, wakimlaki kwa shangwe Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, wakati akiwasili kwenye Uwanja wa Kisiwani, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni za Mgombea huyo leo Septemba 28, 2015. Umati wa Wananchi wa Mji wa Soni katika Jimbo la Bumbuli, wakisikiliza sera za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, wakati Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Kisiwani, leo Septemba 28, 2015. Waziri Mkuu...
Published By: ZanziNews

Kipindupindu chatua Singida, yumo aliyetokea Dar

Wakazi 11 wa Manispaa ya Singida, wamelazwa kwenye kambi ya Mandewa iliyotengwa kwa ajili ya wagonjwa wa kipindupindu, wakihofiwa kuugua ugonjwa huo....
Published By: Mwananchi:

Magufuli: Nakerwa na vigezo vya uzoefu kuomba ajira

Mgombea wa urais kupitia CCM, Dk John Magufuli amesema iwapo atapewa ridhaa ya kuingia Ikulu atapambana kuhakikisha Watanzania wengi wanapata ajira na kwamba anakerwa sana na kigezo cha mtu kuwa na uzoefu ndio apatiwe ajira...
Published By: Mwananchi

NEC yajikanganya

*Mkurugenzi Tehama aondolewa * Maofisa watoa kauli tofauti NA SHABANI MATUTU, DAR ES SALAAM MKURUGENZI wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Dk. Sisti Cariah ameondolewa kwenye nafasi hiyo, imefahamika. Taarifa za uhakika kutoka ndani ya NEC ambazo MTANZANIA ilizipata juzi na jana  zimeeleza kuwa mkurugenzi huyo ambaye ni mtu muhimu katika Tume ameondolewa katika siku za karibuni huku kukiwa hakuna taarifa ya wapi alikohamishiwa   serikalini. Chanzo hicho cha ndani ya tume kimesema  mkurugenzi huyo ameondolewa siku tano zilizopita huku zikiwa zimesalia siku...
Published By: Mtanzania

Post a Comment: