HEKAYA ZA MTAA: UNAPO MAGUFULIKA ILHALI NI MFUASI WA MKWERE
Kumekua na staili mpya ambao ndugu zangu wale wa
kijani na njano wamekua wakiwatambia wale wenzetu wa vidole viwili kwa wiki hii
yote sasa wanaiita magufulika.
Suala lililozua gumzo leo mtaani ni pale wanapoonekana
watu wenye haiba na hulka tofauti na ndugu yetu Magufuli wakisapoti na kushabikia
staili hiyo mpya.
Huku mtaani ikiwa inaaminika ndugu pombe
aliianzisha hii staili kudhibitisha uimara wake wa kutenda kazi na kutimiza
yale anayoyaahidi likiwemo suala la uzembe kazini na mafisadi,lakini hapo hapo
watu wanaonekana kushabikia sana ni sampuli ya wale wale ambao ni wafuasi wa
mkwere,nikimaanisha watu wa maneno mengi ya sio na vitendo (wazembe ) na
wapenda sana kunufaisha matumbo yao binafsi(mafisadi )
Kutokana na hili, swali tulilojiuliza wengi je
magufuli naye ni mkwere!? na kama si mkwere hawa wanamsapoti ilhali wakijijua wao
ni wafuasi wa mkwere wana mpango na ajenda ipi iliojificha !? kuna jamaa yetu
mmoja yeye alienda mbali na kudai ndugu pombe hakua tayari kwa hii kazi na
alikurupishwa ndio maana hana budi kua televisheni inayosubiri amri kutoka kwa
muongozaji mwenye kiongozo.Na ndio sababu wafuasi wa mkwere wanajiamini
hatowadhuru na kumshabikia
Mchangiaji mwingine ambaye alipita tu kutafuna
kashata za jioni jioni yeye alisema kushabikiwa kwa magufulika staili na
wafuasi wa mkwere ni matokeo ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa USEMBA
(upungufu wa sera mbadala ) kwa wana kijani na njano.
Basi mada ilizidi pamba moto ikichochewa na
vijisenti vichache vya malofa kupata gahawa na kashata,ndipo naye muhuza kahawa
akahitimisha mada kwa kuchangia hili “watanzania wa leo wanajua sana kwenda na
mitindo ya kisasa inayokuja kwenye soko,hivyo ukiwaletea magufulika wamo,ukiwambia
wapige kazi wataitika ila na huwezi wabadilisha katika kile wanachokipenda
zaidi ama walichokiamua, hata ukikishusha thamani watakitafuta (ulipo tupo) na
kukithamini hicho chao”hivyo tuwaache wakwere wasapoti magufulika ila siku ya mnada
wa tarehe 25 haitouzika sababu wengi wanaujua ulafi wa wakwere.
Ndipo nami Nilipoamua
kuondoka kuja huku kwenu nako kuwajulisha hekaya za mtaa
Post a Comment: