HEKAYA ZA MTAA: MZEE KIFIMBO CHEZA HUJAMUONA MAGUFULI !?
Naam As-salamu alaykum
waungwana,karibuni tena, tupate kilichojili leo kwenye kijiwe cha mtaa wetu wa
siasa,kama mada inavyowasilishwa kwenu na mwanahekaya mkuu.
Basi leo siku ilikua nzuri kwa watani hawa
wa jadi hapa kitaani,na walianza vyema sana kwa kila mmoja kuiwamba ngozi yake
kwa mafuta aghalabu mno kuyapata hapa mtaani.
Baada ya kila upande kuonesha umaridadi
wa jinsi alivyoiwamba ngozi ya ngoma atakayoipiga kwa msimu wa 2015/20 ndipo
wachangiaji walipoanza toa yao katika kuboresha mashindano.kwa sasa nitaeleza
mchango wa mmoja wa wachangiaji ambaye yeye aliuliza “yuko wapi mzee kifimbo
cheza?”
Binafsi namkumbuka mzee huyu ambaye
alikua mkali sana kwa waharibifu/wachafuzi wa lugha waliongozwa na madenge,
lodi lofa , watoto mapacha na wengineo.hivyo swali lake liliamsha sikio langu
na kutega vizuri kwanini kauliza hivyo.
Ndipo nilipomsikia akianza kulalama,hawa
wajamaa zetu hawana adabu kabisa siku ile jangwani mkuu wao alituita sisi
malofa wao wakachekelea,haikutosha wakaenda karatu wakatufananisha na mnyama
nyumbu asiyeona.yote hayo sisi tumekaa kimya sasa wanamuita mtu aliye hai
marehemu.hivi kweli hawa wanaijua vyema lugha ya Kiswahili !? lakini yuko wapi Yule
mwalimu wa kudhibiti lugha chafu kama hizi za mafisiemu !?
Basi ukimtizama mchangiaji jinsi
alivyokua anaongea kwa hisia hakika lazima aguse hisia za mtima wako,na katika
kuchombeza hili mwenzetu mmoja akaongezea "eeh jamani !!" hivi huyu bwana sijui ana
adabu gani !? maana baada ya kututusi sisi majirani haikutosha sasa ameanza kuwatusi ndugu zake na kuwaita kunguni.kweli ndugu yako unamuita na kunguni !?,na
kama ndugu yako ni kunguni hakika unamaanisha nawe ni wajamii hiyo,je tukuache
uendelee kunyonya damu zetu !? la hasha hapana.
Taharuki kubwa ilitupata ghafla pale
mwenzetu Mwinyimpeku aliposema mzizi ule wa muarobaini mchungu tuliozoea
kutuadhibu kwa zaidi ya miaka 50 pasipo kukatika,dawa yake ni kuumwagia chumvi nyeupe kwenye shina.
Aliposema hayo naaam namimi huyooo
nikamaliza funda langu la tangawizi na andazi nililoshika kisha kunyenyuka
taratibu kuja kuwajuza hekaya za leo,huku moyoni nikijisemea tena “kumbe dawa
ya muarobaini mchungu ni chumvi nyeupe”
Post a Comment: